Sura iliyotangulia

Barua ya muzunguko Juni 1973

“Yesu Kristo ni Yeye yule, jana leo na hata milele” (Waebrania 13:8)

Barua ya muzunguko – Juni 1973

Nawasalimu kwa moyo mkunjufu wasomaji wote wa barua hii, kwa jina la Bwana Yesu Kristo, kwa maneno haya ya Warumi 8:14:

“… kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.“

Kifungu hiki cha maandiko hakitoi tuumuhimu wa imani kwa Bwana Yesu Kristo, lakini pia inazungumuza juu ya uongozi wa Roho Mtakatifu. Sisi sote tunahusika namaneno haya, na tunaalikwa kujijaribu wenyewe. Kumekuwa na watu ambao wanasema wanaongozwa na Roho wa Mungu, lakini kujidai tu hilo haitoshi. Vivyo hivyo, siku hizi tunaona harakati tofauti za kidinizajidai kuwa wamepewa Roho Mtakatifu. Wainjilisti nawahubiri pia wanasema wako chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, na kila mmoja hufanya kile kinachoonekana kuwa kizuri kwake, bila kwelikujinyenyekeza kwa Neno la Mungu, na kwa hiyo, wajiachilie waongozwe na Roho Mtakatifu.

Bila shaka watu hawa, pamoja na harakati hiziza kidini, mara nyingi zilianza katika Roho. Lakini sasa matokeo nigani? Kuanza katika Roho haimaanishi kitu kikubwa, ikiwa uongozi wa Roho Mtakatifu hauendelei mpakahatua ya kutufikisha kwenye ukamilifu.

Paulo anatuonya kwa maneno haya: “Je! Mumekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa katika mwili?” (Gal. 3:3) Kila kitu ambacho niasili ya ki Ungu ni ya kiroho; kwa hivyo, yale yote ambayo watu wanaanza kujiundia wenyewe, hiyo ndiyo mambo ya kimwili. Mmoja anamutenga mwingine, kwa sababu mmoja ametoka kwa Mungu, na mwingine hutoka kwa mwanadamu. Moja huleta uzima, na mwingine, kifo. Kwa sababu: “… kwakuwa nia ya mwili ni mauti, bali nia ya roho ni uzima na amani.” (Rum. 8:6) Ni lazima tutambue kwamba, mbele za Mungu, itastahimili kile tu kilichotungwa na Yeye mwenyewe kwa njia yaRoho wake na kulingana na Neno lake. “Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, namininatenda kazi”. (Yohana 5:17) Hivyo ndivyo Yesu alivyosema, nakatika Wafilipi 2:5 tunapewa onyo hili: Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwemo piya ndani ya Kristo Yesu…” Yule anayebeba ndani yakenia hizoza ki Ungu yeye daima ni pamoja na tendo la Mungu. 1 Wakorintho 2:14 inasema: “Basi mwanadamu watabia yaasli hayapokei mambo ya Roho wa Mungu, maana kwake huyo niupuuzi wala hawezi kuya fahamu, kwakuwa yatambulikana kwajinsi ya Rohoni.” Kila mtu anaweza kujichunguza mwenyewe, nakujuwa kama anapokea kwa furaha Neno lililofunuliwa na Roho wa Mungu, au kama anampinga. Ikiwa kuna upinzani ndani yetu kuhusu Neno la Mungu hapo nikusema kwamba bado tuna nia za kimwili, nakwamba hatuelewi mambo ya kiRoho. Ikiwa kinyume chaketuna nia za kiroho, basi tutajisikiya furaha ya kilindi na hitaji ya kweli ya kupokea chakulakya kiroho.

 

Sura inayofuata