Previous chapter

Barua Ya Mzunguko Aprili / Mei 2019

Salamu za dhati kwa nyote ulimwenguni kwa Jina la thamani la BWANA wetu Yesu Kristo kwa Andiko kutoka 2 Pt 3: 9:

"Bwana hakawii kutimiza ahadi yake, kama wengine wanavyodhani kukawia; bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafilie toba."

Kurudi Kwa Kristo kulikoahidiwa (Yoh 14: 3) ilikuwa ndiyo mada kuu nyakati za kitume, na bado leo kwa waamini wote wa Bibilia. Wakati BWANA alipotabiri uharibifu wa Hekalu katika Mt 24: 1-3, wanafunzi walimuuliza maswali matatu:

1) "Je! Mambo haya yatakuwa lini?
2) Na nini itakuwa ishara ya
kuja kwako ?
3) na ya mwisho wa ulimwengu? "

Kwenye 1 Kor 15, mtume aliandika juu ya ufufuo wa kwanza na ufufuo wa pili na kuelezea: "Kwa kuwa kama vile katika Adamu wote wanakufa, kadhalika katika Kristo wote watahuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake: limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja . Hapo ndipo mwisho… ” (1 Kor 15: 22- 24). Maandiko matakatifu yaneleza kuja kwingi, lakini "Kurudi" ni kumoja tu kwa Kristo (Yh 14: 1-3).

Matendo 3 inasisitiza kile kinachohitajika kutokea kwa kila mmoja kabla ya Kurudi kwa Yesu Kristo kulikoahidiwa: "Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana ; apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa … " (Matendo 3: 19-20). Msamaha mkamilifu wa dhambi na kuhesabiwa haki kukamilifu kwa imani ndani ya ukombozi uliokamilishwa lazima yawe maonjo ya kibinafsi ya kila mmoja ili BWANA atutumie nyakati za kuburudishwa . Uamsho wa kiroho na kuburudishwa ambako BWANA Mungu aliawapa watu wake mwanzoni kwa kumiminwa kwa Roho Mtakatifu kuliahidiwa kwetu pia, kabla ya Kurudi kwa BWANA .

"Ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu. ” (Matendo 3:21). Kurudi kwa Yesu Kristo kunaweza tu kutokea wakati ujumbe ule ule ambao ulitangazwa hapo mwanzo sasa anatangazwa mwisho. Kwa hivyo sio tu juu ya kuburudishwa na ufufuo kwa Roho wa Mungu, lakini juu ya urejesho mkamilifu wa vitu vyote katika Kanisa, kama walivyokuwa mwanzo katika Kanisa la Kwanza, kuhusu mafundisho na hata maisha.

Next chapter