Sura iliyotangulia

Barua Ya Muzunguko no. 23 OKTOBA 1980

“Yesu Kristo ni yeye yule Jana, Leo na Hata milelele”  (Waebrania 13: 8)

Barua Ya Muzunguko no. 23 OKTOBA 1980

Ninawasalimu wote kwa upendo katika Jina la damani la BWANA Yesu Kristo kupitia maneno ya Waebrania 13:20-21:

“Mungu wa salama, ambae alimutowa kati ya wafu ule Muchungaji wa kondoo, kupitia damu ya agano la milele, Bwana wetu Yesu, awafanye wenye uwezo kwa kila tendo njema kwa ajili ya kutimiza mapenzi yake, na atende ndani yenu ambayo imupendezayo, kupitia Yesu Kristo, ambae kwake utukufu milelel na milele! Amen”.

Mungu ni Mungu wa salama, na wale alio wakombowa ni wana wa salama, imeandikwa:

Kwa maana Yeye ni salama yetu, Yeye ambae alifanya wawili kuwa mmoja na akaondowa ile ukuta wa matengano, uadui, ambae kupitia mwili wake akabomoa nguvu za ma agizo na matangazo yake, kusudi ndani yake aweze kuunda mtu mmoja mupya wale ambao walikuwa wawili, akirudisha salama, na kuwapatanisha mmoja na mwengine katika mwili mmoja pamoja na Mungu kupitia njia ya musalaba kwa kubomoa uadui.” (Waefeso 2:14-16)

Hii siyo maneno ya bure ambayo haina maana, ila ni ukweli wa Kiunguambayo inapata zihirisho katika maisha ya wote walio kombolewa. Kupitia njia ya musalaba, uadui na ukuta ya matengano viliondolewa. Ile ambayo ilikuwa inatengenisha iliondoka ikaacha nafasi kwa ile ambayo inaunganisha. Andiko inamanishayale ambayo inasema. Mutu ambae amezaliwa upya ni mutu wa salama; kama mutu si wa salama, ni kusema ya kama hajafanywa upya. Mahali ambapo kweli kweli kazi ya ukombozi iliyomalizika inawekwa pembeni, na kisha ukuesabiwa haki kupitia njia ya sheria inalazimishwa, hapo ndipo uadui ya zamani inaleta mbegu mbaya. Sasa, kati ya wana wa Mungu ugomvi na ubishi; kupitia chuki inaamusha vita kwa namna ambayo haiwezi kuonekana ao kuifikiriwa kwa wale ambao wasiyoamini. Na sasa pale ambapo, kwa imani, kunakuwa pasipo kujizuiza kwa kazi ya ukombozi, hapo Yesu Kristo kama mutetezi anapinga mushitaka wa wandugu. Damu yake inafaa kwa kuunganisha, kusamehe na upatanisho. Watu ambao wamefanywa upya kindani mwao kwa wao wenyewe wanakuwa kweli wapatanishi. Sisi ambao tumepatanishwa na Mungu, tunaweza kujitukuza kwa neema iyoshinda hukumu. Swali la deni yetu imetiwa mara moja wazi. Kwa maana makosa yetu yote imewekwa juu yake; alichukuwa zambi zetu zote; na magonjwa yetu. Yeye ni salama yetu na upatanisho wetu; ndaniya Mwokozi wetu kunapatikana wokovu na uponyaji kwa maana ni wokovu mukamilifu ambayo Mungu alitutolea katika Kristo. Ni Injili inayo dumu siku zote.

Wakati uadui ulikuwa ukifikia shabaa ya mwisho na wakati BWANA alikuwa akiondowa ukuta ya matengano, nguvu za giza zikafika kwa kushambulia, ushambulizi mukubwa juu ya mufalme wa salama. Kusalitiwa ambayo ilitumikishwa, ile hali ya kutolewa katika mikono ya wayuda, mashitaka, ile hukumu, ilekuhayarishwa ilimuleteya kuchukuliwa hata musalabani; aliteswakwa hayo yote bila kufungua kinywa, kama kondoo inayo pelekwa machinjoni. Ila hiyo haikukuwabado mwisho, kwa maana Mungu alikuwa akifuatilia lengo yake mukubwa ya mupango ya wokovu ambayo hata na wafasi wa Yesu hawangeweza kuelewa. Kulikuwa kumeonekana hali moja ambayo ilionyesha namna mambo ingelipashwa kufika. Ndipo sasa, kupitia ufufuko, maisha mapya ikaonekana kwa wale walio kufa katika Kristo na kufufuka pamoja nae. Maisha ya kiungu haiwezi kusimama sababu ya usaliti ao sababu ya kifo ya dunia. Ila maisha ya kiungu ilifunguliwa na ikaja kwa mbegu ya Mungu. Wana na binti za Mungu wana sehemu kwa mateso, kifo, ufufuko, kugeuzwa na kupanda kwa Yesu Kristo. Hakuna mutu ambae anaweza kushindisha mupango ya wokovu ambayo iliyo malizika katika Yesu Kristo. Tunasoma katika 1 Watesalonika 4:14:

Maanaikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao walio lala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye”.

Mungu ni Bwana juu ya maisha na juu ya kifo. Wale ambao wametoka katika mwili katika maisha ya hapa duniani, wanaendelea kuishi kwa Mungu katika hali ya roho. Kupitia damu ya agano la milele, Mungu wa salama alimuleta kutoka wafu Mufalme wa salama, Mufalme muchungaji mukubwa wa kondoo, ambae ni Bwana wetu Yesu Kristo. Roho wa Mungu, ambayo ni nguvu iletayo uzima, haingeweza kumufanya atoke kati ya wafu pasipo damu ya agano la milele kumwangwa kwanza. Na ni hivyo hivyo kwa wale ambao wanakubali zabihu ya kutolewa ya Yesu Kristo pamoja na imani itendayo kazi katika roho. Hatukusulubishwa tu pamoja na Bwana, tumefufuka vile vile pamoja nae kwa ajili ya maisha mapya na kupitia Yeye tunahesabiwa haki kwa hali kamilifu kwa utawa ya kazi ya ukombozi iliyo kamilishwa na Bwana Yesu Kristo. Mutume anaonyesha mawazo ya Mungu kutupatia mazuri yote ifaayo kwa kutimiza mapenzi yake. Ya muhimu katika ufalme wa Mungu, siyo kusema mapenzi ya mwanadamu ifanyike, ila tu mapenzi ya Mungu. Siyo kusema mupango yetu ikamilike, ila mupango ya Mungu iliyo pangwa nae tangu zamani. Ametujulisha mapenzi yake kupitia neno lake lililo funuliwa. Afanye atupatie nguvu ya kulitimiza. Ila inabidi yeye mwenyewe azalishe ndani yetu yale ambayo yana mupendeza. Ni hiyo ndiyo anaweza kutimiza kupitia Roho ndani ya waliyo wake na kupitia hao ambao wataonekana mbele yake. Ndiyo sababu inatubidi tujiweke chini ya uongozi wa roho wake. Hiyo ikuwe ndiyo maombi ya imani yetuambayo inaingia mpaka kwa kiti cha enzi cha Mungu na ikubaliwe nae Mungu mwenyewe, ili atupatie yote ambayo ni mema kwa utimilifu ya mapenzi yake, na atende ndani yetu ambayo inayo mupendeza. Hapo sasa haitakuwa tena mutu, ila Mungu ndani ya Yesu Kristo ambae anapokea heshima ndani ya yote na kwa yote.

 

Sura inayofuata